Wananchi wa Mtwara watahadharishwa na utapeli wa ajira.


Manispaa ya Ntwara Mikindani imewataadharisha wananchi wa wilaya hiyo na maeneo mengine kuwa macho na matapeli walioibuka na kuwatapeli baadhi ya wananchi  fedha kwa madai ya kuwapatia kazi katika manispaa hiyo.
Akizungumza na waandishi wa habari kaimu mkurugenzi na afisa utumishi  wa manispaa hiyo Donald Nsoko amesema utapeli huo kwa sasa ni mkubwa na watu zaidi ya watano wameripoti kuibiwa fedha na matapeli hao hatua iliyowalazimu kufungua jalada polisi lenye namba MT, RB, 36/69 /2015 ili wakamatwe na kutiwa nguvuni.
 
Amesema matapeli hao wamekuwa wakibadilisha majina na kujitambulisha ni afisa utumishi huku wakitumia lugha za kitapeli kuomba fedha kwa minajili ya kuwapatia kazi.
 
Akizungumzia hilo kamanda wa polisi mkoa wa Mtwara Henrry Mwaibambe amekiri kupata malalamiko hayo huku akisisitiza  utapeli huo pia umekuwa ukifanyika katika kiwanda cha dangote kinachozalisha Cementi.
 
Hata hivyo kamanda mwaibambe amewaomba wananchi waliotapeliwa kutoa ushirikiano kwa jeshi la polisi ili watu hao waweze kukamatwa na kutiwa nguvuni.
 
Previous
Next Post »

EmoticonEmoticon

:)
:(
=(
^_^
:D
=D
=)D
|o|
@@,
;)
:-bd
:-d
:p
:ng