Mamlaka
ya udhibiti wa huduma za nishati na maji - EWURA imewataka wamiliki
wote wa matanki ya kuhifadhia mafuta pamoja vituo vya mafuta kutothubutu
kuhodhi mafuta kwa nia ya kuyauza baadaye katika kipindi hiki kuelekea
kuanza kwa utekelezaji wa bajeti mpya ya mwaka 2015/2016 ambayo
inatarajiwa kuanza kutumika julai mosi mwaka huu.
**Kauli
hiyo imetolewa na afisa mkaguzi mkuu wa petroli - EWURA Suleiman Shaban
walipotembelea baadhi ya maghala ya mafuta ili kujiridhisha endapo
nishati hiyo inaendelea kusambazwa kufuatia kuwepo kwa malalamiko kutoka
kwa baadhi ya wananchi kuwa hakuna huduma katika baadhi ya vituo vya
mafuta.
Meneja
uhusiano na mawasiliano Ewura Titus Kaguo amewatoa hofu wananchi
kufuatia ujumbe uliosambazwa kwenye mitandao ya kijamii kuwa nishati
hiyo haitapatikana kwa siku ya jumatatu na jumanne hivyo wanunue mafuta
ya kutosha ambapo amesema taarifa hiyo haina ukweli wowote..
Hata
hivyo kwa mujibu wa Ewura bidhaa hiyo yaweza kupanda katika ya sh.2300
hadi 250 kwa lita kufuatia ongezeko la tozo katika nishati hiyo
iliyopitishwa na bunge lakini pia kupanda kwa dola na kushuka kwa
thamani ya shilingi.
EmoticonEmoticon