TIMU ZA JESHI LA POLISI TANZANIA WAJIFUA MICHUANO YA MAJESHI


xxx
Baadhi ya Wanamichezo wa Polisi walioshiriki Michezo ya Wakuu wa Majeshi ya Polisi kusini mwa Afrika mwaka 2013 nchini Namibia wakiwa katika picha.
Timu za Jeshi la Polisi Tanzania zitakazoshiriki michezo ya Umoja wa Wakuu wa Majeshi ya Polisi kwa nchi za kusini mwa Afrika (SARPCCO), mwishoni mwa mwezi julai nchini Swaziland zinaendelea kujifua vyema katika kambi yao inayoendelea katika chuo cha Taaluma ya Polisi Dar es Salaam (DPA).
Akizungumza na blog hii Mkuu wa kitengo cha michezo cha Jeshi la Polisi, Mrakibu Mwandamizi wa Polisi SSP Jonas Mahanga alizitaja timu zilizopo kambini kuwa ni pamoja na Timu ya Mpira wa miguu, pete, riadha na vishale ambapo hivi sasa zinajifua kuhakikisha kuwa zinakuwa vizuri pindi michuano hiyo itakapoanza kutimua vumbi.
Amesema timu hizo zitaanza kucheza michezo ya kirafiki ili kujipima nguvu na kuhakikisha wanafanya vizuri kwa kuwa michezo ya mwaka huu itakuwa na ushindani mkubwa kutokana na nchi zilizothibitisha kushiriki kujipanga vizuri.
Previous
Next Post »