MCC kudhamini miradi ya umeme mkoani Singida


Mkurugenzi mtendaji wa wilaya ya Ikungi, Bwana Muhammad Nkya akiongea na wataalamu waelekezi wa masuala ya mazingira na jinsia, kutoka kampuni ya CH2M HILL ya Marekani Bi. Cinamon Vann na Bwana Piercarlo Smith (kushoto) walipokuwa mkoani Singida kwa ajili ya upembuzi yakinifu wa miradi ya umeme inayotarajiwa kufadhiliwa na shirika la changamoto za millennia (MCC), makubaliano ya ufadhili wa utekelezaji wa miradi hiyo kwa Tanzania yanatarajiwa kufanyika mwezi Septemba 2015.

Mshauri mwelekezi wa masuala ya jinsia ,kutoka kampuni ya CH2M HILL ya Marekani, Bi. Cinamon Vann (wa pili kulia waliosimama), akiongea na wanawake wa jamii ya kihadzabe na kimang'ati katika kijiji cha kipamba wilaya ya Mkalama mkoani Singida walikokwenda kukusanya taarifa mbalimbali kwa ajili ya upembuzi yakinifu wa miradi ya umeme inayotarajiwa kufadhiliwa na Shirika la Changamoto za Millenia (MCC). Makubaliano ya ufadhili wa utekelezaji wa miradi hiyo awamu ya pili kwa Tanzania yanatarajiwa kufanyika mwezi Septemba 2015.
Mshauri mwelekezi wa masuala ya jamii na mazingira ,kutoka kampuni ya CH2M HILL ya Marekani, Bw. Piercarlo Smith (wa pili kushoto), akiongea na baadhi ya wadau wa mazingira wa halmashauri ya wilaya ya Mkalama mkoani Singida walikokwenda kukusanya taarifa mbalimbali kwa ajili ya upembuzi yakinifu wa miradi ya umeme inayotarajiwa kufadhiliwa na Shirika la Changamoto za Millenia (MCC). Makubaliano ya ufadhili wa utekelezaji wa awamu ya pili wa miradi hiyo kwa Taanzania yanatarajiwa kufanyika mwezi Septemba 2015
Previous
Next Post »