
Kware ni
jamii ya ndege ambao kwa sasa wanafugwa majumbani na wanaotaga mayai
kama kuku ama bata na kwa wingi sana. Ndege hawa ni wadogo 280gm -
300gm, wana rangi ya brown, nyeusi au hata nyeupe yenye miraba na madoa
ya rangi ya udongo au kijivu. Manyoya yao pia yana rangi ya brown au
nyeupe na yenye madoa yanayovutia.
Kutaga na kuatamia
Kware dume humpanda jike kwa muda kidogo, Hapo jike anakuwa tayari kutaga na hutaga mayai 290 hadi 310 kwa mwaka (hii hulingana na lishe nzuri atakayopatiwa).
Kware dume humpanda jike kwa muda kidogo, Hapo jike anakuwa tayari kutaga na hutaga mayai 290 hadi 310 kwa mwaka (hii hulingana na lishe nzuri atakayopatiwa).
Mayai ya Kware huatamiwa kwa siku 18 na huanza kuanguliwa vifaranga kwa muda wa siku 2, kuanzia siku ya 18 na hadi 20.
Njia bora ya kutotolesha mayai ya Kware ni kwa kutumia incubator ambapo mayai huatamiwa kwa wingi ndani ya siku 18.
Utunzaji wa vifaranga na chakula
Siku 1 – 7
Vifaranga
wapatiwe chakula "STARTER PELLET" na maji masafi ya kutosha. Siku ya 1
wawekee 'GLUCOSE' kwenye maji, Packet moja kwa lita 20 za maji, na siku
ya pili hadi ya tano wawekee Amin Total kwenye maji, Wape maji pekee
siku ya sita na siku ya saba wapatie chanjo ya Newcastle. Utawapatia
joto kwa njia ya umeme kwa 'BULB' mbili (2) za 200watts kwa kila
vifaranga 300, ama unaweza kuweka taa ya 'Energy Server' pamoja na jiko
la mkaa uliofunikwa na majivu ambao utakidhi kuwapatia joto sawia kwa
masaa 24 kwa siku 7. (Majivu yanasaidia moto kukaa kwa muda mrefu)(P.T)
Banda/box
lako liwe la ukubwa wa 1.5m x 1.5m (au eneo la ukubwa huo ndani mwa
banda kubwa la kufugia kuku) lazima uzingatie usalama wa vifaranga dhidi
ya panya, paka au vicheche. Unatakiwa kuweka magazeti au mabox chini
kwenye sakafu yatakayosaidia usafi. Kwa week ya kwanza chakula kitawekwa
chini na tunashauri utumie chakula cha pellet ili kusaidia vifaranga
wasiteleze na kuathiri miguu. NOTE: Weka gololi au mawe kwenye drinkers
zako ili kuzuia vifaranga wasizame ndani ya (drinkers) maji na kufa.
Siku 8-14
Vifaranga wataendelea kupewa chakula "STARTER PELLET" na maji safi. Wataendelea kuhitaji 'mwanga' wa kutosha muda wote na joto la wastani bulb 2 za watts 100 au moja ya watts 200
Vifaranga wataendelea kupewa chakula "STARTER PELLET" na maji safi. Wataendelea kuhitaji 'mwanga' wa kutosha muda wote na joto la wastani bulb 2 za watts 100 au moja ya watts 200
Siku 15-21
Uhitaji wa joto utapungua, ila ni kipindi ambacho wanakula chakula zaidi kwa ajili ya kukua. Ni vizuri waendelee kupata taa ili kupata mwangaza utakayowawezesha kula mchana na usiku.
Uhitaji wa joto utapungua, ila ni kipindi ambacho wanakula chakula zaidi kwa ajili ya kukua. Ni vizuri waendelee kupata taa ili kupata mwangaza utakayowawezesha kula mchana na usiku.
Siku 21 na Kuendelea
Kware wako hawatahitaji joto tena wawekee taa tu za energy server kipindi cha usiku, wape chakula na maji ya kutosha zaidi kwa ajili ya kukua.
Kware wako hawatahitaji joto tena wawekee taa tu za energy server kipindi cha usiku, wape chakula na maji ya kutosha zaidi kwa ajili ya kukua.
UTAGAJI MAYAI
WEEK YA SITA
Wiki ya sita kuelekea ya saba Kware wako wataanza kutaga mayai kila siku, kwa wastani Kware mmoja hutaga mayai 300 kwa mwaka.
Magonjwa
Kware ni
ndege wenye kinga kubwa na ni vigumu sana kushambuliwa na magonjwa kama
kuku na mara wanapougua ni rahisi sana kutibika. Magonjwa yanayoweza
kuwapata Kware ni typhoid, mafua na kuharisha .
Tiba za asili
Waweza
kuwatibu vifaranga au Kware wako kwa kutumia njia ya asili ambayo pia ni
rahisi, gharama nafuu na bora zaidi kuliko kutumia madawa
yaliyochanganywa na kemikali na yenye gharama.
Vifuatazo ni vitu vya asili vinavyotumika kutibu magonjwa mbali mbali kwa Kware na yanayopatikana kwa wingi katika maeneo ya mfugaji. Madawa haya hutumika kwa kiwango cha wastani na hayana kipimo maalum kwani hata ukiyazidisha hayana madhara.
Vifuatazo ni vitu vya asili vinavyotumika kutibu magonjwa mbali mbali kwa Kware na yanayopatikana kwa wingi katika maeneo ya mfugaji. Madawa haya hutumika kwa kiwango cha wastani na hayana kipimo maalum kwani hata ukiyazidisha hayana madhara.
Mwarobaini
na Aloe Vera: Madawa haya hutumika kutibu kuharisha damu pamoja na
mafua kwa vifaranga vya Kware. Chukua kiasi kidogo cha mwarubaini kisha
twanga vizuri kupata maji maji. Kamua maji yale, kisha weka katika maji
uliyoandaa kuwanywesha vifaranga wako. Kata vipande vidogovidogo vya
aloe vera (jani moja laweza kutosha) na tia katika maji yaliyochanganywa
na mwarobaini, kisha wapatie vifaranga wanywe (Aloe Vera itaendelea
kujikamua yenyewe ikiwa ndani ya maji huku vifaranga wakiendele kunywa).
Kitunguu
swaumu: Hii hutumika kukinga na kutibu vifaranga vya kware
wanaosumbuliwa na kuharisha damu. Unachukua kitunguu swaumu na kuondoa
maganda ya nje kisha kusafisha na kukata vipande vidogo sana, na
kuwawekea kama chakula. Vifaranga wanapenda sana vitunguu hivyo na
watakula kwa kasi kama chakula lakini ni tiba tayari. Unaweza kuwapatia
kila siku hadi watakapo pona.
Maziwa:Maziwa
yanayotokana na ng'ombe pia hutumika kutibu ugonjwa wa kuhara pamoja na
kuwapa nguvu Kware waliolegea. Mnyweshwe maziwa hayo Kware anayeumwa
bila kuyachemsha na umnyweshe maziwa ya kutosha kiasi cha kushiba.
Unamnywesha mara tatu kwa siku. Hakikisha maziwa unayotumia yanatoka kwa
ng'ombe wanaotibiwa kila mara.
Angalizo
Siyo
lazima Kware waugue ndipo uwapatie tiba hizi. Hakikisha unawapa tiba
kabla hata hawajaugua hivyo utawakinga na magonjwa hayo. Waweza
kuchanganya madawa hayo yote kwa wakati mmoja kwani hayana madhara.
Endapo
madawa ya asili hayapatikani katika eneo la mfugaji basi waweza kuwatibu
Kware kwa madawa yafuatayo ambapo vipimo huelezwa moja kwa moja kwa
maandishi katika madawa hayo au kuelezwa na muuzaji pale utakaponunulia;
Amprolium kwa ugonjwa wa kuharisha damu (Coccidiosis), Fluban,Coridix
au Doxyco kutibu mafua (Coryza) na Esb3,Trisulmycine au Trimazine
hutumika kwa homa ya matumbo (Typhoid).
Chanjo
Siku ya 7 lazima vifaranga wapatiwe chanjo ya "kideri/mdondo"
(respiratory & digestive diseases) kwa dawa inayoitwa 'newcastle'. Chanzo cha maambukizi ni maji na chakula kilichochafuliwa na kinyesi na pia husababishwa na virusi kwa njia ya hewa.
(respiratory & digestive diseases) kwa dawa inayoitwa 'newcastle'. Chanzo cha maambukizi ni maji na chakula kilichochafuliwa na kinyesi na pia husababishwa na virusi kwa njia ya hewa.
Siku ya 14 lazima wapewe chanjo ya "gumboro". Chanzo cha
maambukizi ni maji na chakula kilichochafuliwa na kinyesi na pia husababishwa na virusi kwa njia ya hewa.
maambukizi ni maji na chakula kilichochafuliwa na kinyesi na pia husababishwa na virusi kwa njia ya hewa.
Siku ya
21 lazima warudie chanjo ya "Newcastle (aina ya IBDL)". Chanzo cha
maambukizi ni maji na chakula kilichochafuliwa na kinyesi na pia
husababishwa na virusi kwa njia ya hewa.
Siku ya 35 lazima wapate chanjo ya "Ndui".
Soko
Mayai ya
Kware ni bidhaa adimu sana hapa nchini kwa kuwa ni wafugaji wachache
waliojikita katika ufugaji huu, Ufuatao ni muhtasari wa wastani wa bei
ya bidhaa za Kware sokoni
1. Trei ya (mayai 30) ya KWALE inauzwa shilingi 30,000 .
2. Kifaranga wa Kware wa siku moja anauzwa shilingi 2500 – 3000
3. Kware wa week 4 (mwezi mmoja) anauzwa kwa shilingi 10,000– 12,000
4. Kware aliyeanza kutotoa (week 6) huuzwa shillingi 20,000 – 25,000
5. Kware kwa aliyekomaa kwa ajili ya kitoweo huuzwa kwa shilingi 25,000
6. DROPING za Kware huuzwa kwa shilingi 10,000 kwa 50kg kwa wafugaji wa samaki
2. Kifaranga wa Kware wa siku moja anauzwa shilingi 2500 – 3000
3. Kware wa week 4 (mwezi mmoja) anauzwa kwa shilingi 10,000– 12,000
4. Kware aliyeanza kutotoa (week 6) huuzwa shillingi 20,000 – 25,000
5. Kware kwa aliyekomaa kwa ajili ya kitoweo huuzwa kwa shilingi 25,000
6. DROPING za Kware huuzwa kwa shilingi 10,000 kwa 50kg kwa wafugaji wa samaki
Soko la KWALE liko juu sana kwa mayai na nyama. KWALE pia hutofautiana bei kwa jike na dume.
Mayai yake pia huuzwa kwa bei nzuri sana. Yai moja huuzwa kuanzia 8,000 hadi 12,000 kwa wakati wowote ule.
TUNAKUTAKIA KILA LA KHERI KATIKA UFUGAJI BORA,
KWA MAWASILIANO JUU YA UFUGAJI WA KWARE TEMBELEA UlimwenguWaKware blog
EmoticonEmoticon