Zaidi ya watu 180 wilaya ya sengerema hawana makazi baada ya nyumba zao kuezuliwa na kimbunga.


Zaidi ya wakazi 180 wa kijiji cha mbugani wilaya ya Sengerema mkoani Mwanza hawana makazi baada ya nyumba zao kuezuliwa na kimbunga kilichoambana na mvua kubwa, ambayo pia imeharibu mashamba ya zao la muhogo pamoja na miundombinu ya umeme na barabara.
Jumla ya kaya 33 za vitongoji viwili vya mbugani na CCM katika kijiji hicho zimeathirika kutokana na kimbunga hicho ambapo familia za waathirika kwa sasa zimepatiwa hifadhi ya muda katika nyumba ya diwani wa kata ya bulyaheke bageti nyuti, huku wahusika wakiiomba serikali kuwasaidia mahema pamoja na mablanketi ili kujisitiri na hali ya baridi kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha.
 
Kufuatia tukio hilo uongozi wa serikali ya wilayani Sengerema umeanza kutoa misaada mbalimbali ya vyakula kwa ajili ya waathirika hao, hatua ambayo imeungwa mkono na  watu mbalimbali akiwemo mkazi wa Sengerema Eston Kasika ambaye ametoa kilo 1320 za unga wa sembe, kilo 460 za mchele, kilo 360 za maharage, lita 40 za mafuta ya kula, katoni sita za sabuni za kufuli na katoni moja za sabuni za dawa, kilo 66 za sukari, katoni mbili za chumvi pamoja na dazani 40 za maji makubwa ya kunywa – vyenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni nne.
 
Afisa mtendaji wa kata ya bulyaheke mabula Enock amesema tathimini ya nyumba zilizoezuliwa iliyofanywa na wataalamu wa halmashauri ya wilaya ya Sengerema ni zaidi ya shilingi milioni. 
 
Previous
Next Post »