RPC NGONYANI WA NJOMBE APATA AJALI NA BODYGAD WAKE AFARIKI PAPO HAPO

 Hilo ndio gari la RPC Ngonyani baada ya ajali
Kamanda wa polisi mkoa wa Njombe SACP Fulgence Ngonyani.



Muonekana wa Gari la Kamanda wa Polisi Mkoa wa Njombe BAADA YA AJALI USIKU HUKO TANWATT, KIBENA  Njombe.Picha na Gabriel Kilamlya


Taarifa ambazo zimetufikia katika chumba chetu cha habari muda huu zinasema kwamba kamanda wa polisi mkoa wa Njombe SACP Fulgence Ngonyani amepata ajali mbaya ya gari usiku wa kuamkia leo akitoka Makambako kuelekea Njombe

Kwa mujibu wa taarifa ajali hiyo imesababisha kifo cha "body guard" wa kamanda Ngonyani ajulikanaye kama H580 PC Geroge kufariki dunia papo hapo, huku kamanda Ngonyani na dereva wake Nwaka Seme wakinusurika na kwa sasa wanaendelea na matibabu katika hospitali ya Mkoa wa Njombe

Akizungumza na mwandishi wetu Katika Hospitali ya Mkoa wa Njombe Muuguzi wa Zamu Bi.Neda Chelesi Amesema Kuwa Ajali Hiyo Imetokea Maeneo ya TANWATT Karibu na Jengo la TANSEED Kibena Usiku wa Kuamkia leo Agosti 9 Mwaka Huu na Kwamba Katika Ajali Hiyo Amepokea Majeruhi Wawili na Maiti Moja

Chanzo cha ajali hiyo inayodaiwa kutokea majira ya saa tano usiku hakijafahamika na  taarifa zaidi utazidi  kupata endelea kutufuatilia.

Mtandao huu unawapa pole sana.
Previous
Next Post »