BORA MUHESHIMIWA HUKO NDIKO KWENYE USALAMA

BAADA YA NDOA KUVUNJIKA  VICK KAMATA AJISALIMISHA KWA YESU
Kwa mara ya kwanza Mbunge wa Viti Maalum (UVCCM) Mkoa wa Geita, Vicky Kamata, amekiri kupata pigo mbele ya wachungaji kufuatia ndoa aliyotarajia kufunga Mei 24, mwaka huu kuvunjia.Kamata alitarajia kufunga ndoa na Charles Gadner lakini ndoa ya msanii huyo wa muziki wa kizazi kipya haikuweza kufungwa kama ilivyopangwa awali kutokana na sababu mbalimbali zilizojitokeza siku chache kabla ya harusi hiyo.
''Tukio hilo limenipa fursa ya kujifunza kuwatambua marafiki wa kweli na maaduzi zangu...na wapo waliojipiga vifua wakidai wao ndio wameingilia kuvuruga mpango huo nasema huo ni mpango wa mungu pekee hakuna cha mchawi au adui wala mwanasiasa anayeweza kutekeleza hilo,''alidai Kamata huku akibubujikwa na mchozi.
Katika maandalizi ya harusi hiyo yalidaiwa kuwa ni ya kifahari na yalitajwa kufikia Sh. milioni 96.
Uonavyo wewe Pesa inaweza kununua upendo?
Previous
Next Post »