HABARI MPYA KUHUSU NDEGE YA MALAYSIA AIRLINES ILIYOPOTEA

Eneo jipya la kutafuta ndege ya Malaysia iliyopotea limetangazwa na serikali ya Australia baada ya taarifa mpya za Satellite kutolewa.

Kwa mujibu wa waziri mkuu Warren Truss, zoezi la utafutaji wa ndege hiyo sasa litahamia Kusini kuegemea eneo la kilomita 1,800 kutoka Pwani ya Magharibi ya Australia.
 malay2
Ndege ya MH370 ilipotea wakati wa safari yake kutokea Kuala Lumpur kwenda Beijing Machi 8 mwaka huu ikiwa na abiria 239 ndani yake.
Previous
Next Post »