Neymar Mkombozi: Mbrazil huyo anayevaa jezi namba 10 alifunga mawili.
NYOTA aliyebeba matumaini ya Wabrazil wengi, Neymar amefunga mabao mawili usiku huu katika ushindi wa mabao 3-1 dhidi ya Croatia kwenye mchezo wa ufunguzi wa fainali za kombe la dunia.
Wenyeji walijifunga mapema dakika ya 7 ya kipindi cha kwanza baada ya Marcelo kuujaza mpira nyavuni katika harakati za kuokoa na kuzua ukimya mkubwa uwanjani kwa mashabiki wa Brazil waliofurika kushuhudia timu yao..
Mambo almanusura yawe mabaya kwa Brazil wakati Neymar alipomfanyia faulo mbaya kiungo wa Croatia Luka Modric, lakini mwamuzi Yuichi Nishimura alimzawadia kadi ya njano tu.
Baadaye Neymar alifunga bao la kusawazisha kwa shuti la mbali na aliongeza bao la pili kwa njia ya mkwaju ya penati baada ya mwamuzi kutoa penati yenye utata kufuatia Dehan Lovren kumfanyia madhambi Fred.
Oscar alihitimisha karamu ya mabao kwa Wabrazil na kutoka na ushindi wa kwanza katika michuano ya mwaka huu inayofanyika katika ardhi yao.
![Spot on (just about): Neymar puts his penalty past Stipe Pletikosa despite the Croatia keeper getting a hand to it](https://lh3.googleusercontent.com/blogger_img_proxy/AEn0k_v-KyC9bXOMkfW5Y5gfZJNVOF1HwRMZZNkIFOA3JQARbJu-ILtrzy0Pl0nWOmDkIhbfoDqGqIeMNRw4WoPKpsZEy9o0TGtKrvdag_1NLHYBWGwPlPgBJmtALEjCIPZ32R0Fi7UWbEVezU_9jVhCE1D46dmHrJLsD-VeCJJNMA=s0-d)
Mkwaju wa penati: Neymar alifunga penati yake ingawa kipa wa Croatia aligusa mpira.
Hapa chini ni viwango vya wachezaji wa timu zote na alama zimetolewa juu ya 10.
Neymar ndiye mchezaji bora wa mechi ya leo kwa kupata alama 8 akifuatiwa na Oscar mwenye alama 7.
Kikosi cha Brazil na viwango vyao: Julio Cesar 6; Dani Alves 5.5, Thiago Silva 6, Luiz 6, Marcelo 5.5, Paulinho 6, Gustavo 7, Hulk 6 (Bernard 68), Oscar 7, Neymar 8, Fred 6.5.
Wachezaji wa akiba: Jefferson, Fernandinho, Dante, Maxwell, Henrique, Ramires, Hernanes, Willian, Jo, Maicon, Victor.
Kikosi cha Croatia na viwango vyao: Pletikosa 6, Srna 6.5, Corluka 7, Lovren 6.5, Vrsaljko 6; Modric 7, Rakitic 7, Perisic 6.5, Kovacic 6 (Brozovic 62), Olic 6, Jelavic 6.
Wachezaji wa akiba: Zelenika, Pranjic, Vukojevic, Schildenfeld, Rebic, Sammir, Vida, Eduardo, Subasic.
Anajiangusha chini kirahisi: Fred akianguka baada ya kupewa misukosuko na Dejan Lovren na mwamuzi aliwazadia penati Brazil
Luiz Felipe Scolari akimkumbatia Neymar baada ya kufunga bao la kusawazisha.
Neymar (kushoto)akishangilia bao lake la kwanza
![Left foot forward: Neymar rifles in a shot from outside the box which sneaks into the corner](https://lh3.googleusercontent.com/blogger_img_proxy/AEn0k_uvU3VsRiC8-YleI0JNUQRdvMQbtqNVXvXwtMyLxH7ohe8KcxhjLwVKHrFsr3Kb6SPL9lwGuRWoxqy2_sN9AzfS4vMUkWhek6J4UT6-AD5PQb51ZNxc_ZALKgCkhrYi2tqrDaLKBXh3DevHXn4kzTDOBFD0DJVDEbbyNoZh=s0-d)
Guu la kushoto: Neymar akipiga shuti nje ya eneo la hatari na kuutumbukiza mpira kwenye kona
![Despairing dive: Croatia goalkeeper Stipe Pletikosa fails to save Neymar's effort from the edge of the box](https://lh3.googleusercontent.com/blogger_img_proxy/AEn0k_sTdwNfay8P8Auyw9EvcsVcLNJR69CjbIV0JW3Gte1A0V36RmYBIUnNWGO3X6WVZNPCKqn2zu2xT5dwivRwj2bd8nbNdzPT1dbmo-S8KGjssIVYQs-sBjzZhooBvsysUh5SwXZuzpvdt27Dr3_uSRwgsLhQMwo2FtMFZgoFzw=s0-d)
Kipa wa Croatia Stipe Pletikosa akijaribu kuokoa shuti la Neymar lakini aliambulia manyoya tu
![Long-range effort: Neymar's goal was from well outside the box](https://lh3.googleusercontent.com/blogger_img_proxy/AEn0k_ua1afBzWxdPLM87gG5HY76iDeP2GlIfHzWHwqH5QAuq2PI29FtPEEbta0miJUkPQJjgG4zzPx0KSYenZst8i8noNEjXHcws_Hd_ai4XeYHJkJPXfw_bXsODdqIdI83AW8LCAaKgy0eH3jp5VNvUMeo1oH8upMGcWY7P7jT=s0-d)
Bao la mbali kabisa: Goli la Neymar lilitoka nje ya boksi kama uonavyo kwenye picha ya juu.
![Arrowing in: Neymar's shot was powerful and accurate](https://lh3.googleusercontent.com/blogger_img_proxy/AEn0k_uHJX60cDHI8FPSbqeGEUQE9uSMJb-Yl4HxL4BPxY2rI1Hz4dhWpgMKMKRNFvUhUzTYFdTI2KIuxLJ8R4ef-27s-dwlCGGzw4CabnOtXswyC6cDQ5fMEz3pUQILxwd6fBGObv7wz2n_xbI4qiTh4e_cv1IX1HO_T5Vq5v4yNg=s0-d)
Mshale huo unaonesha jinsi shuti la Neymar lilivyokuwa na nguzu na lililengwa eneo sahihi
![Unexpected: Marcelo (second right) steers the ball beyond his own keeper Julio Cesar](https://lh3.googleusercontent.com/blogger_img_proxy/AEn0k_tJnIX21wdW_0-UAhQPnWbGlB20bJGktmQvTkH2dADWIzP2s2eSiJFxekDSGx16xuPb00m1Cfn8J1ZUORcExPgkk_nE_97VM3_8QQCu_9CF8wUNXWjaNQBIMXjNKQlqnetbxQtK71Ct7VX-iYz5hDphhWlm-XzNg8-I-7dQ=s0-d)
Hakutarajia : Marcelo (wa pili kulia) alijifunga bao na kumwacha kipa Julio Cesar akiduwaa.
EmoticonEmoticon