Wezi wa mifugo weanaoshukiwa kuwa Wafulani wamewaua watu 79 katika kijiji kimoja Kaskazini mwa Nigeria katika jimbo la Zamfara.
Vyombo vya habari nchini Nigeria mnamo Jumapili vilimtaja Msemaji wa Gavana wa jimbo hilo, Bwana Nuhu Salihu Anka, akisema kuwa watu hao waliuawa na watu wanaoshukiwa kuwa wezi wa mifugo kutoka jamii ya Fulani, ambao ni wachungaji.
Maafisa wakuu katika Serikali ya jimbo la Zamfara walihudhuria mazishi ya watu hao 79 katika eneo hilo hiyo jana. Naye msemaji wa polisi wa Taifa, Lawal Abdullahi alisema kuwa watu 30 waliuawa katika shambulio la Jumamosi wakati wachungaji waliokuwa na bunduki kutoka jamii ya Fulani walipovamia mkutano wa wajumbe kutoka Majimbo ya Zamfara, Kaduna, Kebbi na Kastine wakijadiliana changa moto za usalama katika maeneo yao.
Anka anatajwa kusema kwamba wamekuwa wakikabiliana na mashambulizi mabaya sana ya magenge ya watu wenye silaha na wezi wa ngombe lakini shambulio hili la sasa ndiyo baya zaidi.
Kiongozi mmoja wa kijadi amenukuliwa akisema idadi ya waliokufa ni wengi zaidi. Alisema hadi kufikia Jumapili walikuwa wamewazika watu 120 kutokana na shambulizi hilo na kuwa idadi hiyo inatazamiwa kuongezeka zaidi.
Artikel Menarik Lainnya
RC SHIGELLA AWATAKA WENYEVITI WA MITAA KUSIMAMIA KWA UMAKINI SHUGHULI ZA MAENDELEO KWENYE MAENEO YAO Mkuu wa Mkoa wa Tanga,Mh Martini Shigella akizungumza na wenyeviti wa mitaa kuhusu kujadil
More 1 of 358 MKUU WA MKOA WA DAR ES SALAAM, MHE. PAUL MAKONDA AWAPONGEZA KATAA UNENE FAMILY KWA KUADHIMISHA MIAKA 3 Kiongozi wa Kataa Unene Family Bi Angela Msangi (katikati) akiwakaribisha wanachama wenzake w
TAARIFA KUTOKA JESHI LA POLISI MKOANI MBEYA Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya limeendelea kufanya misako, operesheni na doria zenye tija k
More 1 of 376 TAASISI YA KILIMANJARO DIALOGUE YATAKA WANAHABARI KUTUMIA KALAMU ZAO KUDUMISHA AMANI NCHINI Mdhamini wa Taasisi ya Kilimanjaro Dialogue, Habib Miradji (katikati) akiongoza m
SABODO AMSHAURI RAIS MAGUFULI AZIDI KUPUNGUZA BARAZA LA MAWAZIRI Mfanyabiashara maarufu nchini, Jaffar Sabodo akizungumza nyumbani kwake Upanga Dar es Sa
WAZIRI JENISTA ATOA SOMO KWA MABENKI, FINCA YAPETA Sekta za kifedha zinazohusika na utoaji wa mikopo nchini zimetakiwa kutenga utoaji wa m
EmoticonEmoticon