REAL MADRID, CHELSEA ZAFUZU NUSU FAINALI LIGI YA MABINGWA

Defining moment: Substitute Demba Ba slides home Chelsea's second goal to secure a semi-final place
Winner: Demba Ba celebrates after scoring the goal that sent Chelsea into the semi-finals
BAO la dakika ya 88 la Demba Ba limeivusha Chelsea hadi Nusu Fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya kwa faida ya bao la ugenini baada ya sare ya jumla 3-3, usiku huu ikishinda 2-0 Uwanja wa Stamford Bridge, London.
Andre Schurrle alitangulia kuifungia Chelsea dakika ya 32, akimalizia pasi ya David Luiz na baada ya hapo PSG wakawabana The Blues hadi dakika za lala salama Ba alipofanya vitu.
Kocha Jose Mourinho ambaye timu yake ilifungwa 3-1 katika mchezo wa kwanza mjini Paris, Ufaransa alipagawa kwa furaha baada ya bao la Ba akaenda kushangilia na wachezaji wake kwenye kibendera.
Katika mchezo mwingine, Real Madrid imefuzu kwenye tundu la sindano kwenda Nusu Fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya baada ya kuchapwa mabao 2-0 na Borrusia Dortmund usiku huu Uwanja wa Signal-Iduna-Park mjini Dortmund.
Mabao ya Marco Reus dakika ya 24 na 37 yaliwafanya wenyeji waende kupumzika wanaongoza kwa 2-0 na kufanya matokeo ya jumla yawe 3-2 baada ya kufungwa 3-0 katika mchezo wa kwanza.
Missed: Dortmund were left to rue a number of missed chances, including three from Henrikh Mkhitaryan
Katika mechi nyingine, Real Madrid wamefuzu hatua ya nusu fainali licha ya kufungwa mabao 2-0 na Borrusia Dortmund katika dimba la Signal Iduna Park.
Madrid wamenusurika kutokana na ushindi wa mabao 3-o walioupata Santiago Bernabeu katika mchezo wa kwanza.
Real wakianza bila ya Cristiano Ronaldo ambaye hakuwa fiti kuanza mchezo wa leo, walikaribia kutolewa na
vijana wa Jurgen Klopp, lakini jitihada za mlinda mlango wao, Iker Casillas zimewaepushia balaa la kutolewa.
Hata hivyo, Real Madrid walikosa penati baada ya winga wake nyota, Angel Di Maria kuteleza wakati akipiga tuta hilo, hivyo kipa wa Borussia kuokoa kirahisi.
Previous
Next Post »