ANGALIA HII NDIO JEZI MPYA ZA MAN UNITED ZA MSIMU UJAO


HIZI ndizo mpya za msimu ujao za Manchester United?
Jezi mpya za Mashetani Wekundu zimevuja kwenye mitandao ya kijamii, ambazo ni za Nike zikiwa na rangi nyekundu na chata la rangi nyeupe wadhamini wapya, Chevrolet kwa mbele.
Jezi hizo zina zipu nyeusi kutokea shingoni kuelekea chini na ufito mweusi kwenye pindo za mikono na mabegani.
Pamoja na hayo haijathibishwa kama habari kuhusu jezi hizo ni sahihi. United ilitangaza Julai mwaka 2012 udhamini wa jezi na Chevrolet, ambao watakuwa wakilipa Pauni Milioni 25 kwa mwaka kuweka jina lao kwenye jezi za timu hiyo kuanzia msimu ujao. 
Wadhamini wa sasa wa United, Aon, hawataonekana tena kwenye jezi za timu hiyo kuanzia msimu ujao.
Mabingwa hao wa Ligi Kuu ya England wanaweza kuvuna fedha zaidi kutokana na ongezeko la dau la udhamini wa vifaa vya michezo. 
United imekuwa kwenye mazungumzo na Nike kuingia Mkataba wao mpya wa miaka 13, lakini kwa mujibu wa Daily Mail, Wekundu hao wanajiandaa kuingia kwenye miezi mingine sita ya kusaka dili zuri zaidi kabla ya kujitia pingu. Mkataba wa sasa wa Nike unamalizika mwishoni mwa msimu ujao. 
Uwanjani, United inajaribu kufufua makali yake msimu huu baada ya kipigo ambacho hawakutarajia kutoka kwa Olympiacos kwenye Ligi ya Mabingwa Ulaya.
United iliyofungwa kwenye mechi ya kwanza ya Hatua ya 16 Bora mjini Athens, Ugiriki inatumai kuzinduka itakaposafiri hadi Uwanja wa The Hawthorns kesho kumenyana na wenyeji West Bromwich Albion katika mchezo wa Ligi Kuu.
This season's model: United's 2013/14 strip


Robin van Persie wears United's away kit this season
Hawataonekana tena kuanzia msimu ujao: Jezi za sasa za nyumbani za United iliyovaliwa na Wayne Rooney (kushoto) na za ugenini iliyovaliwa na Robin van Persie (kulia) 
All white on the night: United's third kit is this white number
Jezi ya tatu ya United
Previous
Next Post »