MWILI WA WAZIRI WA FEDHA KUWASIRI KESHO JUMAMOSI DAR



Mwili wa aliekua Waziri wa fedha na Uchumi Dr. William Mgimwa unatarajiwa kuwasili Dar es salaam Tanzania kesho Jumamosi Jan 4 2014 ukitokea Afrika Kusini kwenye hospitali aliyokua kalazwa.

Mwenyekiti wa kamati ya kitaifa ya mazishi ambae ni Waziri wa nchi ofisi ya Waziri mkuu sera uratibu na bunge William Lukuvi amesema baada ya kuwasili Jumamosi hiyohiyo saa tano asubuhi ataagwa kwenye viwanja vya Karimjee Dar es salaam kabla ya kusafirishwa kuelekea Magunga Iringa kwa maziko January 6.


Previous
Next Post »