WILAYA YA MBARALI – KUINGIA NCHINI BILA KIBALI.
MNAMO
TAREHE 02.12.2013 MAJIRA YA SAA 07:50HRS HUKO KATIKA KIJIJI CHA
KIJIJI CHA LEMBUKA- IYAMBOGO, KATA
YA CHIMALA,
TARAFA YA ILONGO WILAYA YA
MBARALI MKOA WA MBEYA.
ASKARI POLISI WAKIWA DORIA/MSAKO WALIWAKAMATA 1. BERETE S/O TEFRA, MIAKA
24, 2. SAMWEL S/O GIRMA, MIAKA 30 NA
3. MUATU S/O BALAGALA, MIAKA 23 WOTE
RAIA NA WAKAZI WA NCHINI ETHIOPIA
WAKIWA WAMEINGIA NCHINI BILA KIBALI. MBINU
NI KUSAFIRI KWA NJIA YA KIFICHO. TARATIBU
ZA KISHERIA ZINAFANYWA ILI WAKABIDHIWE IDARA YA
UHAMIAJI. KAIMU KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA KAMISHNA MSAIDIZI WA
POLISI BARAKAEL MASAKI ANATOA WITO KWA JAMII KUENDELEA KUTOA TAARIFA KATIKA MAMLAKA HUSIKA JUU
YA MTU/WATU WANAOWATILIA SHAKA IKIWA NI
PAMOJA NA RAIA WA KIGENI ILI UCHUNGUZI DHIDI YAO UFANYIKE NA HATUA ZA KISHERIA
ZICHUKULIWE DHIDI YAO IKIWA NI PAMOJA NA KUKAMATWA.
[BARAKAEL MASAKI - ACP]
KAIMU KAMANDA WA
POLISI MKOA WA MBEYA.
EmoticonEmoticon