Muimbaji mahiri wa Zimbabwe Chiwoniso Maraire afariki dunia.

Chiwoniso

 Mmoja wa waimbaji maarufu wanaofahamika nchini Zimbabwe Chiwoniso Maraire amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 37.

Albam aliyoitoa Chiwoniso iliyoitwa ‘Ancient Voices’ ilimfanya kuwa staa katika dunia ya muziki katika miaka ya 1990.

Alikuwa akipiga ‘mbira’ au ‘thumb piano’ chombo ambacho nchini humo ni wanaume tu pekee kitamaduni ndio waliokuwa wakitakiwa kukipiga.

Amefariki kwa kile kunachihisiwa kuwa ni ugonjwa wa Nimonia, ikiwa ni mwaka mmoja tu tangu kifo cha aliyekuwa mume wake Andy Brown, ambaye pia alikuwa mwanamuziki mahiri.

Wanandoa hao wa zamani wameacha watoto wawili.

Chiwoniso alikuwa binti wa mwanamuziki anayeheshimika Zimbabwe kwa kupiga ‘Mbira’ Dumisani Maraire, aliyefundisha katika Chuo Kikuu cha Zimbabwe.

Hakupata tu heshima kwa kuwa alivunja mwiko kwa kupiga ‘mbira’ lakini pia kwa kufanikiwa kuuchanganya sauti za asili za Zimbabwe na vyombo vya kisasa.

Alizaliwa marekani mwaka 1976 na baadae kurejea nchini kwao Zimbabwe akiwa na umri wa miaka 7.

Previous
Next Post »