Na Lilian Mkusa, Njombe
WIKI iliyopita katika Mtaa wa Maheve uliopo
Kata ya Ramadhani mkoani Njombe yalitokea mauaji ya kutisha
yanayomhusisha mtoto aliyemkatakata mama yake mzazi kwa shoka kutokana
na kugombania mirathi.
Baada ya kufuatilia kisa hicho cha kutisha,
kwa kuwasiliana na ndugu wa marehemu, Serikali ya Mtaa na taarifa kwenye
mazishi ya mama huyo, Ferejina Mligo (65), Daraja Letu limesimuliwa
namna kijana alivyomtoa mama yake roho.
SeMlowe, ambaye ni binamu wa
marehemu, anaeleza kuwa kijana huyo, Fiano Mgeni (26) alifanya kitendo
hicho cha kinyama Jumatatu Mei 20, 2013, nyumbani kwao Mtaa wa Maheve.
“Fiano
alimvamia mama yake na kuanza kudai kuwa kwa nini ameuza eneo la
familia lililokuwa na milingoti mitatu bila taarifa?”anasema SeMlowe.
Inaelezwa
kuwa, mama huyo alijaribu kujitetea kwa kueleza kuwa suala hilo tayari
lilishajadiliwa kifamilia na kufikia muafaka, lakini kijana huyo
aliendelea kumfokea na kumpiga na shoka katika maeneo yake ya mwili.
“Tulikuwa
kijiweni ghafla Fiano akaja na akawa anajitapa kwamba ameua, amemaliza
kazi kwa manufaa ya wengi,” anasema mmoja wa wakazi wa eneo hilo ambaye
hakutaka jina lake litajwe.
Grewn Mtulo, Ofisa Mtendaji wa Kijiji cha
Maheve, amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kwamba mpaka sasa
mtuhumiwa anashikiliwa na polisi huku taratibu nyingine zikiendeelea
kufuatiliwa.
“Suala hili ni zito, tutaandaa mkutano wa hadhara
tuzungumze na vijana juu ya tabia hizi za kikatili zinazoendelea kwa
sababu zinaturudisha nyuma kimaendeleo,” anasema kiongozi huyo.
Next
« Prev Post
« Prev Post
Previous
Next Post »
Next Post »
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
EmoticonEmoticon