Waziri
wa Habari Vijana, Utamaduni na Michezo Dkt. Fenella Mukangara (pichani)
amewashauri vijana nchini kushiriki kambi ya Dunia ya vijana
inayotarajia kufanyika mwishoni mwa mwezi huu katika ukumbi wa Mlimani
City jijini Dar es Salaam.
Waziri
Dkt. Mukangara ameutoa ushauri huo hivi karibuni wakati akiongea na
vijana wa kikundi cha Mambo Safi kilichopo Kata ya Kimara jijini Dar es
Salaam.
Amesema
kuwa vijana kushiriki kwao katika kambi hiyo kutawawezesha kujifunza
mambo mengi ikiwa ni pamoja na utamaduni wa watu kutoka nchini Korea na
China, pia watakutana na watu kutoka mataifa mbalimbali ambapo wataweza
kubadilishana mawazo na hivyo kujengeka kifikra.
Kwa
upande wake Viola Massawe kutoka International Youths Fellowship
(IYF) amesema kuwa malengo waliyonayo ni kuwakutanisha vijana 2000
katika maudhui ya badilisha FIKRA kutoka mtazamo hasi kwenda mtazamo
chanya pamoja na tamasha la Muziki wa Cantata.
Massawe
amesema kuwa mshiriki wa mkutano huo ambaye ni kijana anatakiwa kulipia
kiingilio cha shilingi 10,000/= kwa gharama hizo atapataT-shirt,
kitabu , chakula na malazi kwa muda wa siku tano na cheti pindi
atakapomaliza mafunzo.
Amesema
“Kutakuwa na hotuba na mafundisho kuhusu elimu ya ufahamu, tamasha la
muziki za Gracias kwaya, michezo ya utamaduni ya kimataifa, masomo ya
Academy kwa lugha za Kispanish, Kichina, Kirussia, Kikorea, Kiingereza,
TAE-KWON-DO na Marathon”.
Kambi
hiyo inaandaliwa na Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo kwa
kushirikiana na International Youths Fellowship (IYF) itaanza tarehe 29
Julai, hadi tarehe 2 Agosti mwaka huu.
Kambi
ya vijana imekuwa ikifanyika nchini kuanzia mwaka 2009 kwa mwaka jana
vijana 1000 kutoka pande zote za Tanzania waliweza kushiriki huku wengi
wao waliweza kuishi maisha mapya kupitia kambi ya IYF kwa kupewa fikra
ya maana na mtazamo chanya juu ya mambo ya maisha yao.
EmoticonEmoticon