Afghanistan yamtimua kazi Waziri wake wa Mambo ya Ndani.

132973163_afghan_434152c

 Bunge la Afghanistan  limemfukuza kazi Waziri wa Mambo ya Ndani Mujtaba Patang (pichani), ambaye ni mmoja wa wakuu wa usalama nchini humo, ikiwa haujatimia ya mwaka mmoja tu baada ya kuchukua wadhifa huo.

Patang ameondolewa kupitia hoja ya kutokuwa na imani naye iliyopigiwa kura 136 dhidi ya 60, kuhusiana na shutuma za ufisadi na kuzembea kazini katika makabiliano na wanamgambo wa Taliban.

Waziri Mkuu huyo ameachishwa kazi ikiwa ni mwezi mmoja baada ya serikali ya Aghanistan kuchukua rasmi majukumu ya usalama wa nchi kutoka kwa majeshi ya Jumuiya ya Kujihami ya NATO yanayoongozwa na Marekani.

Bunge lilimwondoa mtangulizi wa Patang, Bismillah Mohammadi mnamo Agosti 2012, kwa kudaiwa kushindwa kuitisha uasi wa wanamgambo wa Taliban pamoja na mapigano ya mpakani kati ya nchi hiyo na Pakistan.

Previous
Next Post »