KINANA AMPA RUNGU FILIKUNJOMBE ATAKA AENDELEE NA MOTO WA KUWAPIGANIA WANANCHI WAKE



katibu  mkuu  wa CCM Taifa  Bw Kinana  Kushoto) akiwa na mbunge  wa  jimbo la Ludewa  Deo Filikunjombe leo jimboni Ludewa
..................................................................................................................................................... 
WAKATI  kukiwa na  tetesi  za chini  kwa  chini ndani ya  chama  cha mapinduzi (CCM) kuwa  chama  hicho kimekuwa  kikiwachukia  wabunge wa CCM wanaokishambulika  chama  hicho  bungeni akiwemo mbunge  wa  jimbo la Ludewa Deo Filikunjombe na mbunge wa  jimbo la Mwibara Kang Lugola ambao  wamekuwa wakiipinga  serikali ,katibu mkuu  wa CCM Taifa  Abdulrahman Kinana amempongeza  mbunge  huyo na kumtaka aendelee na moto huo huo  wa  kuwapigania  wananchi  wake.
Hata  hivyo kabla ya  Kinana  kumpa rungu mbele ya  wsananchi mbunge Filikunjombe wananchi wa  jimbo  hilo walionyesha  kumbana  kiongozi huyo kwa  kuhoji  sababu ya wabunge  wa CCM bungeni  kufanya kazi ya kukipongeza chama  chao  huku  wengi  wao  wakiwa kimya (mabubu) katika  kuchangia na  wale  wanaochangia kama mbunge  wao Filikunjombe  wamekuwa  waklichukiwa kuwa ni  wapinzani ndani ya CCM . 
Hivyo  wananchi hao  kumweleza katibu mkuu  huyo aliyeongozana na katibu wa itikadi na uenezi  wa CCM Taifa  Nape Nnauye  kuwa wao  wataendelea  kumuunga mkono mbunge Filikunjombe kwa  vipindi  vingine  tena tena  vitatu vya miaka 15  tena  hadi mbunge mwenyewe  atakapoamua  kuacha  kugombea na iwapo watafanya mchezo  basi wao watamfuata  mbunge  huyo kokote atakakokuwa.
" Mheshimiwa  tunaomba  leo chama kitueleze  hivi  kwanini wabunge wa CCM wamekuwa  si msaada kwa wapiga  kura  wao muda  wote  wamekuwa  kimya  bungeni na  wale  wanaochangia  wanachangia kupongeza  chama .....sasa  tunaomba  kukueleza  kuwa sisi  tupo na mbunge  wetu  na hata  wana  CCM wanaojipitisha jimbo la Ludewa  wakiamini  sisi tutayumba  uwaeleze  kuwa CCM hatudanganyiki  "
Akizungumza jana  na  wananchi  wa  wilaya ya  Ludewa ambao  walikusanyika kwa wingi katika mkutano  wa hadhara  kwa lengo la kutaka  kusikia kauli ya CCM juu ya uamuzi  utakaochukuliwa kwa mbunge   wao kutokana na kuwepo kwa kauli  za chini kwa chini katika jimbo  hilo kuwa ziara ya Kinana jimboni  humo ni kutaka  kumshughulikia mbunge  huyo.
Akizungumza na  wananchi hao Kinana  alisema  kuwa lazima  wabunge  wa CCM kuiga mfano  wa Filikunjombe kwa  kuwasemea  wananchi  waliowachagua  na kuwa mbunge ambae  amekuwa hawasemei  wananchi  wake  bungeni hatoshi  kuwa mbunge . 
Hivyo  kuwataka  wananchi  kuwa makini kwa kuwaangalia  wabunge  wao  waliowachagua kuona  kitu gani  wanakifanya  bungeni na  kuwahukumu  kulingana na kile  wanachokifanya kama  hawawasemei  kuwa nao makini. 
Hata  hivyo Kinana aliwataka  wananchi hao  wanaounga mkono uamuzi  wa kuendelea  kumwongeza muda wa vipindi  vitatu Filikunjombe  kunyosha  mikono  juu na baada ya  wananchi  wote  kunyosha  mikono yao  juu alisema pia kwa upande  wake anaungana na wao na kuwa chama hakitafanya makosa kwa  kuwasaliti  kuwapa mtu mwingine katika  uchaguzi ujao wa mwaka 2015 . 
"Hata  mimi katibu  mkuu naungana na uamuzi wenu wa  kumwongeza muda Filikunjombe na  napenda  kuwahakikishia  kuwa CCM haitafanya makosa  itaendelea  kuwaachia Filikunjombe kama mlivyomchagua wenyewe  labda ashindwe  yeye " 
Katika  hatua  nyingine  Kinana alisema  kuwa CCM hakitafanya makosa  katika  kuwateua  wagombea wa nafasi mbali mbali na kuwa  watakaoendelea  kuteuliwa ni wale ambao  wanafanya  vizuri katika majimbo yao. 
Aidha  alikiri utendaji kazi  wa mbunge Filikunjombe na  kuwa ni m bunge  wa mfano katika  bunge na kuwa  hata  chama  kinapendezwa na uchapakazi  wake na  kuwa mbali ya  wananchi  wa  jimbo  hilo kumwita ni jembe  ila yeye kama Kinana anamfananisha mbunge  huyo na katapila kwani amekuwa hamwogopi mtu  katika utendaji kazi wake. 
Pia  alisema  kuwa  mbali ya Filikunjombe  kufanya kazi  vema  ila bado ni kijana anayejituma na  pia ni kwa kiasi ni mbabe katika kupigania  wananchi  wake .
Kuhusu shughuli  za kimaendeleo  zinazofanywa na mbunge huyo Kinana  alisema  kuwa wao kama  chama wanapendezwa na kazi  za mbunge  huyo na kuwa  toka anaanza  ziara ya  siku mbili hakuna hata  sehemu moja ambayo wanampinga  mbunge  huyo .
Awali akiwa katika  kata ya Mlangali wananchi  wa eneo  hilo walimkana mbunge wa  viti maalum mkoa  wa Njombe na mjumbe  wa kamati kuu  ya  CCM Taifa Pindi Chana kuwa hawamtambui mbali ya  kuuwakilisha mkoa  huo wa Njombe.
Wananchi hao  walimkana mbunge  huyo baada ya Kinana kuwauliza kama wanamtambua mbunge  huyo. 
Kwa  upande  wake Filikunjombe alisema mbali ya  kuanza mradoi mkubwa wa lami katika wilaya  hiyo ila bado kuna mradi  wa maji wenye thamani ya Tsh bilioni 1.5 ambao utaondoa adha ya maji katika  mji  wa Ludewa. 
Filikunjombe  alisema  kutokana na kuendelea  kuutamani ubunge  wake ataendelea  kuwatumikia vema  wananchi na kamwe siku  zote hatarudi nyuma bungeni katika  kuwapigania  wananchi hao .
Previous
Next Post »