AUA KINYAMA MPENZI WAKE KWA WIVU WA KIMAPENZI

 
 
Maiti ya Mwanamke Uliokotwa kwenye mashamba ya mkonge Mkoani morogoro hivi karibuni baada ya  kujinyonga (picha na maktaba)
 
Mrembo mmoja  mkazi  wa Ihanzutwa  wilaya ya Mufindi  mkoani  Iringa  Neema Kisanga ( 35) ameuwawa  kinyama na mpenzi  wake  baada ya  kupigwa na kitu kizito  kichwani na kupelekea  fuvu la kichwa kupasuka kabla ya  kunyongwa  shingo.
 
Habari  kutoka wilayani Mufindi ambazo zimethibitisha na  viongozi  wa serikali ya kijiji  hicho  zinadai  kuwa  tukio  hilo May 11 mwaka  huu katika  kijiji  hicho.
 
Imedaiwa  kuwa  mwanamke  huyo alikutwa na mauti hayo akiwa nyumbani kwake majira ya saa 6 usiku baada ya  mpenzi  wake aliyejulikana kwa jina la Edward Mdegella kumvamia na kuanza kumpa kichapo hadi  kusababisha kifo chake.
 
Mashuhuda hao  walioteta na mtandao  huu  wa www.matukiodaima.com  wanadai  kuwa chanzo cha ugomvi huo uliosababisha kifo  cha mrembo huyo ni  wivu  wa kimapenzi na baada ya  kufanya mauwaji hayo mtuhumiwa alitoweka  kusiko  julikana
 
Source:Francis Godwin
Previous
Next Post »