Moshi mweusi ukiashiria hakuna papa mpya aliyechaguliwa siku ya kwanza baada ya makardinali kujifungia katika hekalu maalum, huko Vatican City |
Makardinali katika ibada katika kanisa la St. Peter Basillica kabla ya kujifungia kumchagua Papa hapo jana |
Zoezi
la kumchagua papa atakayeongoza kanisa Katoliki duniani lilianza hapa jana
Vatican City kwenye jumba maarufu la Sistine Chapel ambalo hutumika kwa ajili
hiyo.
Makardinali
wapatao 115 akiwepo Mudhama Policarp Kardinali Pengo wa Tanzania ni miongoni mwa
walikusanyika kufanya zoezi hilo.
Yoyote
kati ya makardinali hao anaweza kuwa papa mpya hivyo Kardinal Pengo naye ana
nafasi ya kuwa papa mpya baada ya Papa Benedict xiv ambaye amestaafu.
Kwa
sasa Papa Benedict amepewa jina jipya na ataitwa Papa Emaritus au Papa Emeritus
wa Roma.
Kinachosubiriwa
hapo kwa sasa ni moshi mweupe ambao ndio utakaonyesha papa mpya amepatikana na
kama hajapatikana baada ya kupiga kura moshi mweusi utaonekana.
Makardinali
hao watakaa katika jumba hilo hadi papa apatikane. Hawaruhusiwi kuwasiliana na
mtu yoyote na watakuwa wakipiga kura mara nne kwa siku.
Mudhama Policap Kardinali Pengo (kulia) leo hii akiwa na Makardinali wenzake Vitican City |
Mudhama Policap Kardiali Pengo kushoto akiwa na mmoja wa makardinali hapo jana mjini Vatican |
EmoticonEmoticon