Yule mwanamke wa Sudan aliyehukumiwa kifo kwa kukana dini yake,ameachiwa huru.



mwanamke

Kwa mujibu wa BBC, Mwanamke wa Sudan aliyehukumiwa kifo kwa kosa la kuikana imani ya dini yake na kuolewa na mwanaume anayempenda wa kikristu amechiwa kutoka gerezani.

 Shirika la habari la Suna limeripoti kuwa, hukumu ya kifo iliyotolewa kwa mwanamke huyo Meriam Ibrahim ilibadilishwa na mahakama ya rufaa.

 Mwanamke huyo aliolewa na mwanaume wa kikristu na alihukumiwa kifo kwa kutumia sheria za kiislamu baada ya kukataa kurejea kwenye dini yake.

 Mume wake amesema kuwa anatarajia kumuona mke wake akirejea nyumbani.

 Aliwekwa gerezani tangu February mwaka huu akiwa na mtoto wake mdogo wa kiume aliyejifungua akiwa ndani.
Previous
Next Post »