Watano wauwawa kwenye shambulizi lingine la tatu Kenya

Watu watano wanadaiwa kuuawa katika shambulizi lilifanywa na kundi la watu wenye bunduki katika eneo la Pwani ya Kenya, karibu na eneo la Mpeketoni ambalo wiki yalifanyika mashambulizi mawili yaliyosababisha vifo vya watu 60.
Kwa mujibu wa BBC, maafisa wameeleza kuwa watu wenye silaha walivamia kijiji cha Witu, kilichoko kilometa 15 kutoka mji wa Mpeketoni, Jumanne alfajiri (Leo).
Hakuna kundi lililodai kuhusika na shambulizi hili la tatu.
Kundi la Al-Shabab lilidai kuhusika na mashambulizi mawili ya wiki iliyopita katika eneo la Mpeketoni karibu na Lamu.
Hata hivyo, rais Uhuru Kenyatta alipinga na kudai kuwa mashambulizi hayo yanatokana na uchochezi wa wanasiasa wapinzani
Previous
Next Post »