Na Saimeni Mgalula,Mbeya
Hali si swali kwa MKUU wa Wilaya ya Mbarali Gulamu Hussen Kiffu
kunusurika kuumizwa na wanafunzi wa Chuo cha Uuguzi cha Chimala
kilichopo Wilayani humo mkoani hapa baada ya kuvamia gari lake na
kuvunja vioo,kutoa upepo wa matairi kutokana na Serikali kufunga chuo
hicho kwa kutokuwa na hadhi ya kudaili wanafunzi, watu watano
wamefikishwa mahakamani.
Kutokana na vurugu hizo zilizotokea chuoni hapo jana jioni, Jeshi la
polisi Mkoani hapa linawashikilia wanafunzi sita akiwemo Mkuu wa
Chuo hicho Francis Mtega kwa tuhuma za kuhamasisha vurugu
zilizopelekea kuharibu gari la Mkuu wa Wilaya ya Mbarali.
Kamanda wa polisi Mkoani hapa Diwani Athuman alisema baada ya mkuu
wa wilaya kuongozana na baadhi ya viongozi wa serikali hususani
kamati ya ulinzi na usalama wilaya kwa lengo la kutaka kujua sababu za
chuo hicho kuendelea kufundisha wakati serikali ilitoa agizo kifungwe
ndipo hapo walipovamiwa na wanachuo hao.
Alisema tukio hilo lilitokea muda mfupi baada ya kuwasili Chuoni
hapo kwa lengo la kuzungumza na uongozi wa chuo ndipo baadhi ya
wanafunzi walivamia gari la Mkuu wa Wilaya na kuanza kuvunja vioo kwa
kutumia mawena kisha kutoa upepo kwa malengo yasiyojulikana.
Kamanda Athumani alisema tukio hilo linaonesha ni mpango uliokuwa
umepangwa na uongozi wa Chuo kwa muda mrefu kwani serikali ina
malengo mazuri kwa watanzania na lengo kuu ilitaka chuo hicho
kisajiliwe ili kitambulike na Serikali na kuweza kutoa wauguzi walio
na sifa na kuwawezesha kupata ajira itakayotambulika serikalini.
Aliongeza kuwa kitu cha kushangaza ni madaraka aliyonayo mkuu wa chuo
hicho ambapo yeye mwenyewe ni mwalimu na mhasibu na kwamba kulikuwa
hakuna sababu ya kufanya vurugu bali kilikuwa ni kitu cha kutoa
vielelezo vya udaili wa chuo.
Alisema katika uchunguzi wa awali umebaini kuwa chuo hicho kimeanza
muda mrefu na tayari kimeweza kutoa wauguzi katika Nyanja mbalimbali
bila ya serikali kutambua kama hakijasajiliwa na hakitambuliki.
Next
« Prev Post
« Prev Post
Previous
Next Post »
Next Post »
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
EmoticonEmoticon