TAARIFA YA ULINZI NA USALAMA KANDA NO.02 MKOA WA MBEYA TAREHE 21/10/2013.


         
S/N
Tarehe
Muda
Maelezo ya  kosa/Tukio
Watuhumiwa
1.
20.10.2013
09:00hrs
MB/IR/9307/2013 – MAUAJI.
Huko katika Kijiji cha Mjele, Kata ya  Mshewe, Tarafa ya  Utengule – Usongwe  Wilaya ya Mbeya Vijijini    Mkoa wa Mbeya.  FRANK S/O WILLIAM, miaka 30, Msafwa, mkulima na mkazi wa Mjele aliuawa kwa kupigwa sehemu mbalimbali za mwili wake na kundi la wananchi walioamua kujichukulia sheria mkononi wakitumia silaha za jadi fimbo na mawe. Chanzo cha mauaji hayo ni tuhuma za wizi baada ya  marehemu kukutwa akiwa ameiba  kuku watatu mali ya  DISMAS S/O RASHID. Mwili wa marehemu umefanyiwa uchunguzi na kukabidhiwa ndugu kwa mazishi. Upelelezi unaendelea kuwabaini na kuwakamata waliohusikana na tukio hili.
       ----
2.
19.10.2013
20:30hrs
KYL/IR/2360/2013 – MAUAJI.
Huko katika Kijiji cha Lupembe, Kata ya Katumba Songwe, Tarafa ya Unyakyusa, Wilaya ya Kyela    Mkoa wa Mbeya. GODFREY S/O MWAKAPILA, miaka 21, Kyusa, mkulima na mkazi wa Kijiji cha Mpunguti aliuawa kwa kupigwa sehemu mbalimbali za mwili wake na kundi la wananchi walioamua kujichukulia sheria mkononi wakitumia silaha za jadi fimbo na mawe. Chanzo cha mauaji hayo ni tuhuma za wizi wa ng’ombe mmoja mali ya MOTO S/O MWAKIANGE, miaka 36, Kyusa, mkulima, mkazi wa Kijiji cha Muungano ambaye amekamatwa kwa mahojiano. Mwili wa marehemu umefanyiwa uchunguzi na kukabidhiwa ndugu kwa mazishi. Upelelezi unaendelea kuwabaini na kuwakamata watu wengine waliohusikana na tukio hili.
         01.








B: Idadi ya watendaji.
Ø  Jumla ya askari 1,401 waliingia kazini, doria na malindo mbalimbali.
Ø  Jumla ya  watumishi raia waliopo ni  21.
Ø  Jumla ya  vikundi vya ulinzi jirani ni 240,  jumla ya  vikundi vilivyoshiriki  ni  101  na walinzi   381  walishiriki katika doria/malindo mbalimbali.
Ø  Jumla ya  askari Mgambo waliopo ni 790
Ø  Jumla ya Polisi wasaidizi waliopo ni 420.
C: Mafanikio yaliyopatikana.
§  Mafanikio yaliyopatikana kupitia doria,misako na operesheni ni kama ifuatavyo:-
v  Bhangi – Nil
v  Dawa za kulevya {drugs} – Nil
v  Pombe ya Moshi -Nil
v  Mirungi – Nil
v  Silaha – Nil
v  Nyara za Serikali – Nil

D: Ukamataji wa makosa ya Usalama barabarani.
§  Jumla ya  makosa yaliyokamatwa – 91
§  Kesi zilizopelekwa Mahakamani – Nil
§  Jumla ya  tozo [Notification] Tshs  2,430,000/=

E: Watuhumiwa waliokamatwa kwa makosa mbalimbali.

  • Jumla ya watuhumiwa waliokamatwa ni 18.
  • Wahalifu wazoefu {Harbitual } – Hakuna.
  • Wahalifu waangaliwa {Supervisee} – Hakuna
  • Waliofungwa {Convicted}-  Hakuna.
  • Wahalifu waliachiliwa huru {Acquited}- Hakuna.

Nawasilisha tafadhali.    
                   
                                                             [P.A. MHAKO – ASP]
              Kny:                KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA.
Previous
Next Post »