Mtanzania Zinduka...!
Na:
Meshack Maganga-Iringa.
Nimemaliza kusoma
kitabu cha ‘Success Principles’ Kilicho andikwa na Jack Canfield, kwenye kitabu
hiki nimejifunza kwamba, ukitaka kufanikiwa kwenye mambo yako lazima utambue
kwamba wewe ndiye mkurugenzi mtendaji wa
maisha yako, mazingira, mifumo, familia na vikwazo vyovyote duniani visiwe
sababu ya kuutuliza utu wako. Unazo nguvu zaidi ya nguvu zilizo nje yako za
kuwa unavyotaka, kulingana na jinsi ulivyojaliwa. Vipo vitu vinavyoweza
kukuzuia hata kukumaliza lakini ni uamuzi wako kusimama kidete kwaajili ya
maisha yako na kuonyesha nguvu zilizo ndani yako au kukubali kumalizwa bila
ubishi wowote.
Mwanzoni mwa mwaka huu, nilibahatika kusoma makala ya mwandishi maarufu Freddy Macha
kwenye gazeti la Mwananchi yenye kichwa ‘Maisha
Bongo,Majuu hali moja’. Kwenye makala yake Freddy Macha alilezea waziwazi
kwamba wapo baadhi ya vijana wa kibongo ambao huota kwenda kuishi ‘majuu’ bila kujua kwamba huko maisha
ni magumu kuliko hata bongo,na kwamba, popote pale unapoishi utawakuta watu
wakilalamika na kusema kuwa afadhali kwenda mahali pengine. Kisha akaenda mbali
kwakusema kuwa, ukijua na kutambua la kufanya na namna ya kumudu
maisha,unaendelea na mapambano,kwa sababu kanuni kuu ya uhai ni harakati.
Kwenye makala zangu
mabalimbali mimi na Albert Sanga, tumekuwa tukiwaelezea watanzania wenzetu juu
ya kuwekeza kwenye kilimo cha miti, mboga na matunda na ufugaji wapo walio
elewa na wapo wanaolalamika umbali wa masaa mawili kutoka sehemu wanayoishi
mpaka mashambani. Na wapo wanaoona kwamba kilimo ni kazi za watu duni,
walioshindwa shule, nk. Na wapo ambao wameamua kuwa wanaharakati wa kusifia
maisha ya wacheza mpira wa ligi za ulaya na kupoteza muda vijiweni.
Kwenye makala yake, Albert Sanga yenye kichwa
WATANZANIA NA ARDHI alisema, Jambo jingine linalotumaliza watanzania ni
kutokuwa na maono ya muda mrefu. Wengi wetu tunataka mambo ya papo kwa papo,
hatupendi kuangalia mambo ya vipindi virefu mbele. Mfano mzuri ni katika hili
la uwekezaji katika ardhi.
Mtu anaona ni
kupoteza fedha kununua shamba leo ambalo pengine linaweza kuja kutumika miaka
ishirini huko baadae. Mtu anaona ni kama kupoteza fedha kupanda miti leo ambayo
atakuja kuivuna miaka saba ama miaka kumi ijayo.
Wasichokumbuka wengi ni kuwa unachopuuza kufanya leo kwa gharama ndogo
miaka ishirini ama kumi ijayo hutakuwa na uwezo wa kukifanya hata kama
ukitamani.
Kwa bahati nzuri zaidi,
wataalamu wa masuala ya utambuzi na mafanikio na wajasiriamali maarufu hapa
Tanzania na kwingineko duniani kama John Gray, Vincent Peale, Robert Kiyosaki, Donald Trump, Jack
Canfield, Anthony Robbins na wengine, wanabainisha vigezo ambavyo vinaweza
kumfanya mtu kutabiri kama maisha yake yatakuwa ni ya kushindwa hadi mwisho au
yatakuwa ni ya mafanikio.
Mwana mama Rhonda Byrne
kwenye kitabu chake cha ‘The Secret’ ameeleza kwamba, kama mtu akiwa anaamini
kwamba kuna watu wengine wa aina fulani mahali fulani, ambao ndio peke yao
wanaoweza kufanikiwa na kufika juu kwenye ngazi ya kimapato, mtu kama huyo
hawezi kamwe maishani mwake kuja kutoka kwenye lindi la umaskini.
Rhonda, ambae aliishi
maisha ya hali ya chini nayakutisha,anafafanua kwamba, mtu akiwa na mtazamo
huo, hawezi kutoka kwenye lindi hilo kwa sababu juhudi zake ambazo
zingemfikisha mbali zinakuwa tayari zimewekewa mipaka na imani hiyo, kwamba yeye
hahusiki katika kufanikiwa, bali kuna
wengine ambao ni Mungu mwenyewe
anayewajua na aliyewateua. Kwa kufikiri hivo, juhudi yake kubwa katika kutafuta itakuwa ni ile ya kumfanya
asife tu kwa njaa na siyo kuvuka hapo. Kama ujuavyo, tunapoamini kuhusu jambo
Fulani, mawazo yetu hutusaidia kulifikia jambo hilo.
Kuna mwandishi wa
kitabu cha Jitambue enzi zile 2006 nikiwa bado mwanafunzi wa sekondari aliwahi
kuandika kwamba, ‘Hata kama “fuko la fedha” litadondoshwa miguu mwetu
tutalipiga teke na kuliambia “mimi sikuandikiwa kupata bwana, kuna wenyewe,
hali kama hii hujitokeza mara nyingi sana maishani mwetu.”
Tunakabidhiwa dhamana kubwa ambayo
ingetusaidia sana maishani mwetu, lakini tunacheza nayo hadi inapotea kwa
sababu tu hatuamini kwamba utunastahili kuitumia kufika juu. Tunaziona nafasi
za kusonga mbele, lakini tunaamini kwamba, hatustahili kuzitumia.
Fursa zikija waziwazi
kabisa, tunajifanya hatuzioni kwa kutafuta visingizio mbalimbali ili
tusizitumie, kwa sababu tu, tumeamini kwenye mawazo yetu kwamba, sisi
hatustahili.
Ni vigumu kugundua
kwamba nafasi au fursa hizo zimekuja kwa sababu tayari tumejifungia njia
kuelekea mafanikio. Wengine kwa bahati mbaya wanaweza kuona na kubaki
wameshangaa ni kwa nini tushindwa kuinuka katika mazingira tuliyomo.
Mtu anapoamini kwama
hawezi, anayaambia mawazo yake ya kina yamsaidie kumfanya ashindwe zaidi kwenye
kila jaribio analofanya. Badala ya kufanya juhudi kujisaidia ili amudu,
hujipweteka kwa kuamini kwake kwamba hata kama atafanya kitu gani, kamwe
hatamudu. Siyo rahisi kwa mtu mwenye mawazo ya aina hii kuweza kufanikiwa
maishani.
Kuna watu ambao kwa
sababu ya kukosa kile ambacho jamii inakiona kuwa ndiyo ufunguo wa mafanikio,
huwa wanaamini kwamba hawawezi kufanikiwa au kufanya vizuri maishani kama hao
ambao wanacho. Kwa mfano, kwa kukosa elimu, ujuzi au utaalamu fulani, watu
wengine hujihesabu kama wanyonge. Huchukulia kwamba ni wale tu wenye elimu,
ujuzi na utaalamu fulani ndiyo wanaoweza au wanaotakiwa kufanikiwa.
Bila shaka umeshawahi
kusikia au hata wewe mwenyewe kusema, “Si wamesoma bwana’ ndiyo wanaojaliwa,
sisi ambao hatuna elimu kazi yetu itakuwa ni kuwatumikia. Kauli kama hizi zina
chimbuko lake mbali sana, pengine katika malezi yetu. Wazazi kwalizoea au
wamezoea kuwaambia watoto wao, “Usiposoma kazi yako itakuwa ni kuwabebea
wenzako mizigo, unafikiri pesa inaokotwa, nk.
Kwa bahati mbaya mtoto aliyelishwa “sumu” (‘EARLY CHILD PROGRAMMING’) hii anaposhindwa shule, huamini kwamba
yeye atabaki kuwatumikia wengine tu.
Tunapoamini kwamba kwa
sababu hatuna elimu ya kutosha na pengine ujuzi au utaalamu fulani, hatuwezi
kufika juu kwenye mafanikio, tutakuwa tunatafuta kufulia( ama vifafa vya
kiuchumi). Moja ya vigezo muhumu vinavyoweza
kutufikisha kwenye mafanikio ni kuamini kwetu kwamba tunaweza kufika
huko. Tunapokuwa hatuna imani kwamba tunaweza kufika huko hujifungia njia
wenyewe.
Baadhi yetu kuwa
tunaamini kwamba tuna mikosi, balaa au nuksi napengine laana ambazo zinatuzuia
katika kufikia malengo yetu. Tunaamini hivyo kiasi kwamba hata tukifikia karibu
kabisa na mafanikio huwa tunajiambia ni kazi bure, tutaporomoka tu. Na kweli
kwa kuamini hivyo hujikuta tukiporomoka kila tukifika karibu na kufanikwa au
kufikia malengo.
Kinachotokea ni kwamba,
kwa kuamini kwetu kuwa tunamkosi, balaa, laana au nuksi, huwa tunatenda kwa
mkabala huo wa kinuksi au kibalaa na kimkosi, ambapo matokeo yake ni
kujikwamisha. Watalaamu wa elimu ya mafanikio wanaeleza kwamba tunapoamini kuwa
tuna mkosi au nuksi huwa tunayashauri mawazo yetu ya kina kutusaidia kuendelea
kuwa katika hali hizo (Niliwahi kufafanua zana hii nilipoandika
makala ya BINADAMU NI ZAIDI YA MWILI WAKE). Ndiyo maana siyo
rahisi kukuta mtu anayeamini katika
nuksi akiondoka katika hali hiyo.
Tufanyeje basi, kama ni
kweli kimapato tuko hoi napengine tunachoweza ni kupata riziki yetu ya kila
siku tu? Pamoja na kwamba mengi yameelezwa
tayari kwenye mada nyingine, bado tunaweza kukuambia, tunachotakiwa
kufanya ni kujenga imani ya kumudu. Kamwe hatutakiwi kabisa kujiambia tulipofikia
ndipo basi, hatuwezi kupanda zaidi.
Yupo mjasiliamali
fulani,ni dada mpambanaji (Elizabeth Samoja) kwenye ujasiriamali alipata
kuandika hivi, maisha ya
kijana wa kitanzania aliyechagua kuishi Dar es salaam baada ya kumaliza masomo
yake ya chuo kikuu huwa hayaelewiki,(ingawa kwa mtazamo wake yanaeleweka)
utashangaa kijana huyu anapomaliza chuo anaanza zungusha cv ndani ya bahasha ya
kaki,mtaa kwa mtaa,jingo kwa jingo,atapata kazi kampuni ya simu,au bank,au
kampuni ya bia, atapanga chumba mitaa ya
sinza, wengine huchukua mkopo na
nunua gari aina ya vitis,corora,corona,
opa, ama gari lolote lisilozidi milioni
kumi, ataoa amakuolewa,atafanya shopping Mr Price, mjanja mwingine
atakopa hela za kwendea ‘sendoff’ na wengi wao wakijitahidi hununua mariedo,
atavaatai kubwa na kuonekana smart, ataenda club, kuponda raha...
Ukiungalia mlolongo huu vizuri,shughuri nyingi hapo kati zote zinachukua pesa mfukoni mwa ila chanzo cha pato lako ni kimoja tu(ajira), kwa kifupi wewe ni mtumiaji tu....kutoboa kimaisha kwa kufuata mpango huu ngumu sana................
Imefika hatua mpaka mabenki wamejua watanzania si entrepreneurs na investors wanapenda magari ya bei chee,na akijitahidi basi apate nyumba bunju,mbagala,au kitunda.....ndo maana mikopo mingi ya benki wanatangaza kwa kuonyesha nyumba ama gari....maana huko ndo kwenye urahisi na kuna soko na wateja wakubwa maarufu kama ‘victim society’ market. Mtanzania Zinduka......
Usiseme hakuna pesa, pesa zipo nyingi sana, fursa za kumwaga, nina mshangaa huyu mhitimu wa chuo kikuu akiwa mtaani asijue cha kufanya badala yake anaingia kwenye mitandao ya kijamii kama ‘Face book na kuanza kumwaga lawama kibao,jiulize umefanya nini,kwani ulikuja duniani ili ubebwe na serikali? Kwa sasa Tupo watanzania milioni 44 wote tukisubiri kubebwa tutakuwa taifa la aina gani hili?
Ukiungalia mlolongo huu vizuri,shughuri nyingi hapo kati zote zinachukua pesa mfukoni mwa ila chanzo cha pato lako ni kimoja tu(ajira), kwa kifupi wewe ni mtumiaji tu....kutoboa kimaisha kwa kufuata mpango huu ngumu sana................
Imefika hatua mpaka mabenki wamejua watanzania si entrepreneurs na investors wanapenda magari ya bei chee,na akijitahidi basi apate nyumba bunju,mbagala,au kitunda.....ndo maana mikopo mingi ya benki wanatangaza kwa kuonyesha nyumba ama gari....maana huko ndo kwenye urahisi na kuna soko na wateja wakubwa maarufu kama ‘victim society’ market. Mtanzania Zinduka......
Usiseme hakuna pesa, pesa zipo nyingi sana, fursa za kumwaga, nina mshangaa huyu mhitimu wa chuo kikuu akiwa mtaani asijue cha kufanya badala yake anaingia kwenye mitandao ya kijamii kama ‘Face book na kuanza kumwaga lawama kibao,jiulize umefanya nini,kwani ulikuja duniani ili ubebwe na serikali? Kwa sasa Tupo watanzania milioni 44 wote tukisubiri kubebwa tutakuwa taifa la aina gani hili?
meshackmaganga@gmail.com 0767
48 66 36/ 0713 48 66 36.
EmoticonEmoticon