Tetemeko la ardhi lauwa zaidi ya watu 50 nchini China na kusababisha nyumba kadhaa kuporomoka.

0007a50c-642

 

Takribani watu 54 wameuawa na wengine zaidi ya 3,000 wamejeruhiwa kufuatia tetemeko kubwa la ardhi lililotokea katika eneo la milima la magharibi mwa China.

Tetemeko hilo lenye ukubwa wa 6.6 katika kipimo cha richta limepiga karibu na mji wa Dingxi mkoa wa Gansu na kusababisha uharibifu mkubwa wa majumba na kukata huduma za umeme.

Afisa mmoja wa eneo hilo amesema zaidi ya majumba 21,000 yameharibiwa vibaya na takribani 1,200 yameporomoka.

Mkoa wa Ganzu, ambao ni eneo lenye milima, jangwa na malisho ya mifugo, una jumla ya idadi ya watu milioni 26 ukiwa ni moja ya mikoa yenye watu wengi zaidi nchini China.

Shirika la Msalaba mwekundu la China limesema linapeleka katika eneo hilo mahema, vifaa vya matumizi ya nyumbani pamoja na makoti ya baridi na pia linayatuma makundi ya waokoaji kusaidia katika shughuli za kutoa msaada kwa waathiriwa wa tetemeko hilo.

Previous
Next Post »