
 Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini IGP 
Said Mwema, akimkabidhi zawadi yenye nembo ya Jeshi Polisi Tanzania, 
Naibu Kamishina wa UNAMID Dkt. Syed Kaleem Imam, kutoka nchini Sudan, 
jimbo la Darfur, alipomtembelea ofisini kwake Makao Makuu ya Jeshi hilo 
jijini Dar es salaam, akiwa katika ziara yake ya kikazi ya siku sita 
hapa nchini.

Naibu Kamishina wa UNAMID Dkt. Syed
 Kaleem Imam, kutoka nchini Sudan, jimbo la Darfur (wapili kutoka 
kulia), akitoa mada katika kikao cha kubadilishana uzoefu 
kilichowashirikisha makamishina na maofisa waandamizi wa Jeshi la Polisi
 Nchini. Kutoka kulia ni Kamishina wa utawala na fedha wa jeshi la 
polisi, CP Clodwig Mtweve, Kamishina wa Operesheni na Mafunzo wa Jeshi 
la Polisi, CP Paul Chagonja, Mkuu wa tathmini na ufuatiliaji Naibu 
Kamishina wa Polisi (DCP) Omar Rashid pamoja na Mkuu wa Utawala na 
rasilimali wa jeshi la Polisi (DCP)Thobias Andengenye.
EmoticonEmoticon