Waziri Mhagama akikagua maandalizi ya kuadhimisha Sherehe za Miaka 53 ya Muungano katika viwanja vya Jamhuri  leo Mjini Dodoma.
 Baadhi
 ya wananchi wakifuatilia maonesho ya maandalizi ya Maadhimisho ya miaka
 53 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar yanayotarajiwa kufanyika 
terehe 26 Aprili Mjini Dodoma kwa mara ya kwanza tangu Serikali 
ilipohamia Dodoma.
 Vikosi
 vya Ulinzi na Usalama vikiwa kwenye gwaride la maandalizi ya 
maadhimisho ya Maadhimisho ya miaka 53 ya Muungano wa Tanganyika na 
Zanzibar yanayotarajiwa kufanyika terehe 26 Aprili Mjini Dodoma.
 Vikosi
 vya Ulinzi na Usalama vikiwa kwenye gwaride la maandalizi ya 
maadhimisho ya Maadhimisho ya miaka 53 ya Muungano wa Tanganyika na 
Zanzibar yanayotarajiwa kufanyika terehe 26 Aprili Mjini Dodoma.
 Vikosi
 vya Ulinzi na Usalama vikiwa kwenye gwaride la maandalizi ya 
maadhimisho ya Maadhimisho ya miaka 53 ya Muungano wa Tanganyika na 
Zanzibar yanayotarajiwa kufanyika terehe 26 Aprili Mjini Dodoma.
 Askari wa Pikikipi maalum wakionesha namna pikipiki hizo zitakavyopamba maonesho hayo.
 Makomandoo
 wa Jeshi la wananchi wa Tanzania wakionesha umahiri wao wa kuvuta gari 
lenye tani 7 ikiwa ni moja ya mbinu ya medani katika uwanja wa 
mapambano.
 Askari wa Kikosi cha Farasi wakionesha umahiri wao katika kutumia farasi kupambana na uhalifu.
Wanafunzi wa halaiki wakipita kwa ukakamavu mbele ya Jukwaa Kuu.
Na. Immaculate Makilika- MAELEZO - DODOMA
Waziri
 wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Uratibu, Ajira na Wenye 
ulemavu, Jenista Mhagama amewaasa Watanzania kuwa wazalendo pamoja na 
kudumisha amani na utulivu uliopo nchini.
Akizungumza,
 leo mjini Dodoma wakati akifuatatilia maandalizi ya Maadhimisho ya 
miaka 53 ya Muungano yatakayofanyika Aprili 26 mwaka huu katika Uwanja 
wa Jamhuri uliopo mjini Dodoma.
“Tunapoadhimisha
 miaka 53 ya Muungano ninawaomba watanzania kuwa wazalendo pamoja na 
kulinda amani ya nchi” alisema Waziri Mhagama
Pia, 
Waziri Mhagama aliwaomba watanzania hasa wakazi wa Dodoma kuhudhuria kwa
 wingi katika Maadhimisho hayo yatakayofanyika jumatano wiki hii.
Kwa 
upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Jordan Rugimbana alisema kuwa mkoa 
wake umejipanga vizuri katika kufanikisha maadhimisho hayo, ambapo pia 
alivishukuru vyombo vya habari kwa kuhamasisha wananchi juu ya 
maadhimisho hayo.
“Wananchi
 wamehamasika kushiriki katika maadhimisho haya ya miaka 53 ya Muungano,
 ninawashukuru kwa kazi kubwa mliyoifanya na tunaamini mtaendelea 
kuhamasisha wananchi kushiriki katika maadhimisho hayo” alisema 
Rugimbana
Maandalizi
 ya Maadhimisho ya miaka 53 ya Muungano yamehudhuriwa pia na Mkuu wa 
Wilaya ya Dodoma mjini Christina Mndeme, pamoja na viongozi mbalimbali 
wa Serikali.
Aidha,
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli 
anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika maadhimisho hayo, ambapo pia 
yatahudhuriwa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi 
Dkt. Ali Mohammed Shein na viongozi mbalimbali wa dini na Serikali.
Maadhimisho
 hayo ya miaka 53 ya Muungano yanatarajiwa kupambwa namaonesho kutoka 
kutoka vikosi mbalimbali vya ulinzi na usalama, burudani za vikundi vya 
ngoma pamoja na maonesho ya halaiki.

EmoticonEmoticon