Juma Kaseja rasmi Mbeya City, asaini miezi Sita


Baada ya ukimya wa muda mrefu, hatimaye mlinda mlango  maarufu nchini Tanzania ,Juma Kaseja Juma  amesaini  rasmi kuwa  mchezaji wa timu ya Mbeya City ya Jijini Mbeya kwa mkataba utakao muweka jijini Mbeya kwa miezi sita, ambapo ada ya usajili huo ikiwa haijawekwa hadharani 
Kaseja aliyewahi kucheza vilabu vya Moro United, Simba na Yanga kwa vipindi tofauti. Alikuwa nje ya uwanja kwa kipindi kirefu toka alipojiweka kando na mabingwa wa soka Tanzania Bara, timu ya Yanga Sc, na kufuatiwa na misuguano ya kimkataba baina ya pande hizo mbili.
Previous
Next Post »