Mkuu wa wilaya ya Mbeya Nyeremba Munasa akifunga mafunzo ya siku mbili kwa waandikishaji wa daftari la kudumu


Mkuu wa wilaya ya Mbeya  Nyeremba Munasa  akifunga

mafunzo ya siku mbili kwa waandikishaji wa daftari hilo la kudumu yaliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa shule ya sekondari ya Mbeya Day iliyopo Jijini hapa.Picha Jamiimojablog.


Washiriki wa mafunzo ya zoezi la uandikishwaji kwa mfumo wa compyuta wakimsikiliza kwa makini Mkuu wa wilya ya Mbeya Nyirembe Munasa katika ukumbi wa shule ya sekondari ya Mbeya Day jijini Mbeya Mei 18 mwaka huu.





Vifaa vitakavyo tumika katika zoezi la uandikishwaji wa daftrai la kudumu la wapiga kura


Afisa mwandikishaji Msaidizi jimbo Ndugu Vicent Msolla akizungumza katika mafunzo hayo.







Wito umetolewa kwa waandikishaji  wa daftali la kudumu la mpiga kura kwa kutumia mfumo mpya wa  Biometric Voter Registration (BVR), kupuuza kauli za baadhi ya  watu  ambao wanaweza kujitokeza na kutumia kauli za vitisho vya kisisa au vya kigaidi katika zoezi la uandikishaji wa wapiga kura .



Kauli hiyo imetolewa jana na Mkuu wa Wilaya ya Mbeya Nyerembe Munasa, wakati akifunga  mafunzo ya siku mbili kwa waandikishaji wa daftari hilo la kudumu yaliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa shule ya sekondari ya Mbeya Day iliyopo Jijini hapa.



Mkuu huyo wa wilaya amesema nivema wataalamu hao wakatambua kuwa  baadhi ya watu wanaweza kutoa vitisho mbalimbali kwa watu ili wasijiandikishe hivyo ni vema wakawa makini katika kutoa elimu kwa walengwa waweze kujiandikisha.





Aidha, kiongozi huyo aliwasihi wataalamu hao kutojiingiza kwenye matatizo ya kuboresha au kuongeza vitu ambavyo havihusiki kwenye mfumo huo ambao serikali umeufanyia utafiti wa kutosha na kujihakikishia ya kwamba mfumo huo umekidhi viwango vya ubora.



Alisema, Taifa linapenda  kuona nchi inakuwa na mshikamano, tunaingia kwenye uchaguzi  tukiwa salama na tunatoka tukiwa salama na yote haya yatafanikiwa endapo waandikishaji hao watatumika vizuri.



Aidha,  aliwataka kuzingatia ukusanya taarifa mbalimbali za uhalifu na kuzifikisha kwenye mamlaka husika za dola  hususani wageni wanaoingia nchini kinyume cha sheria.



Hata hivyo, Munasa aliwaomba wananchi kujitokeza kwa wingi katika kujiandikisha kwani wataisaidia nchi kupata viongozi sahihi kwa ngazi ya Uraisi, Ubunge na Udiwani.
Mwisho
Previous
Next Post »