KANGE LUGOLA ASEMA NITAKUWA WA MWISHO KUISALITI RASIMU YA WARIOBA


nyalandu_95dc3.jpg
Mjumbe wa Bunge la Katiba, Kangi Lugola ameapa kuwa atakufa na tai shingoni kwa kuitetea hotuba ya Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Joseph Warioba kwa kuwa ndiyo iliyobeba mawazo ya watu wengi.
Kutokana na hilo, Mbunge huyo wa Jimbo la Mwibara anaonekana kutofautiana waziwazi na Mwenyekiti wa chama chake cha CCM, Rais Jakaya Kikwete ambaye aliipinga baadhi ya vipengele vya rasimu hiyo.
Akizungumza baada ya kupangwa kwenye kamati, Lugola alisema kuwa haoni tatizo katika hotuba ya Warioba na kwamba atakuwa wa mwisho kuisaliti.
Alisema kuwa mawazo ya Tume ya Jaji Warioba ndiyo mawazo ya Watanzania walio wengi ambao walipendekeza kuhusu Katiba wanayoitaka.
"Sasa mkisema napingana na Mwenyekiti wangu, nadhani siyo dhambi kufanya hivyo kama tunapingana kwa misingi ya hoja, lakini msimamo wangu mimi ni Serikali tatu ambayo ndiyo hotuba ya Warioba aliyesimama pale kwa niaba ya watu wote," alisema Lugola.
Previous
Next Post »