Timu
ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) inaondoka Mwanza keshokutwa (Julai
24 mwaka huu) kwenda Kampala, Uganda kwa ajili ya mechi ya marudiano ya
Kombe la CHAN itakayochezwa Jumamosi (Julai 27 mwaka huu) Uwanja wa
Mandela kuanzia saa 10 kamili jioni.
Taifa
Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager iko kambini jijini
Mwanza chini ya Kocha Kim Poulsen tangu Julai 14 mwaka huu, kujiandaa
kwa mechi hiyo itakayoamua ni timu ipi kati ya hizo mbili itacheza
Fainali za CHAN zitakazofanyika mwakani nchini Afrika Kusini.
EmoticonEmoticon