BREAKING NEWSSSSSS BASI LA KAMPUNI YA SUMRY KUTOKA MPANDA LAPATA AJALI MBAYA

Ikiwa ni wiki moja sasa toka Basi la SUMRY la Mpanda kupata ajali mbaya na kusababisha Vifo vya watu 9 na kujeruhi wengine zaidi ya 20 na ikiwa ni siku takribani 4 ndani ya wiki moja Basi jingine la SUMRY linalofanya safari zake Kati ya Mbeya - Sumbawanga kupata ajali ,mzimu wa ajali waendelee kuyakumba mabasi ya SUMRY baada ya Leo tena kutokea ajali ya tatu ikiwa ni wiki moja pekee. Ajali hiyo imetokea mchana wa Leo mida ya Saa 8 mchana Katika eneo la Mbuga Yeupe Katika barabara kuu ya Mpanda- Sumbawanga huku ikidaiwa kuwa dereva aliyesababisha ajali hiyo ni Yule aliyesababisha ajali juzi Katika basi la SUMRY linalofanya safari zake Kati ya Mbeya - Sumbawanga . Katika ajali ya Leo inadaiwa hakuna mtu yeyote aliyepoteza maisha.

KWA TAARIFA ZAIDI ENDELEA KUFUATILIA MTANDAO WETU.
Source: www.matukiodaima.com
Previous
Next Post »