WAZIRI MKUU MSTAAFU MH. EDWARD LOWASSA AKABIDHIWA TUZO MKOANI IRINGA

 

IMG_2175
Picha .Askofu wa kituo cha maombezi na uponaji cha Overcomers Power Center (OPC) Dkt Boaz Sollo (kushoto) akimakabidhi tuzo ya heshima mfano wa ramani ya Tanzania waziri mkuu wa zamani Edward Lowassa katika hafla ya kuchangia ujenzi wa kanisa na kuendeleza kituo cha radio Overcomers Fm ,katika harambee hiyo Lowassa aliahidi kuachangia milioni 15 na kufanikisha kupata Tsh zaidi ya milioni 75 zikiwemo fedha taslimu na ahadi IMG_2184
Na Francis Godwin
WAZIRI mkuu mstaafu Edward Lowassa amesema kuwa mbali ya kuwa yeye si tajiri ila bado ataendelea kufanya kazi yake kwa ukaribu zaidi na jamii ikiwa ni pamoja na kushirikiana na marafiki zake kusaidia na kuwataka wale wote wenye kusema dhidi yake kuendelea kusema ila hatarudi nyuma katika kutoa misaada kama njia ya kutafuta baraka za Mungu.
Lowassa ambae pia alikabidhiwa tuzo ya heshima kwa ajili ya kuendeleza kulipigania Taifa la Tanzania ,huku mwenyewe akichangia kiasi cha Tsh milioni 15 na mbunge wa jimbo la Ludewa Deo Filikunjombe akichangia milioni 9 kati ya fedha zote zaidi ya Tsh milioni 75 zilizochangwa kwa ajili ya kuendeleza ujenzi wa kanisa la OPC mkoani Iringa kama njia ya kuhamasisha amani katika Taifa ametaka watanzania kuwapuuza wale wote wanaoeneza siasa za uchochezi .
“Nataka kuwaomba leo wachukieni wachochezi na pia niwaelezeni kuwa mimi si tajiri ila nina utajiri wa watu na ushawishi na ninafanya mambo haya ili kumbukumbu yangu iweze kuandikwa Mbinguni na nimekuwa nikialika watu wengi na nimekuwa nikifika wacha wenye kusema waseme watasema ila usiku watalala wenyewe ….sitaacha kusaidia kwa kuogopa kusemwa”
Previous
Next Post »