SHEIKHE PONDA APANDISHWA KIZIMBANI MAAHAKAMA YA HAKIMU MKAZI MOROGORO LEO

 
  Sheikh Issa Ponda akiwa mahakani mkoani Morogoro  leo asubuhi .
 
Sheikh Ponda amesomewa mashtaka matatu katika mahakama ya morogoro likiwemo la uchochezi  kwenye mkutano wa hadhara uliofanyoka ogasti 10 ambapo inadaiwa alisema 'Ndugu  waislamu msikubali uundwaji wa kamati za ulinzi na  usalama za misikitini kwani kamati hizo zimeundwa na Bakwata ambao ni vibaraka wa serikali'
  
Sheikh Ponda amefikishwa mahakamani hapo chini ya ulin zi mkali akisindikizwa na msafara wa magari yaliyokuwa na polisi. Ponda amesafirishwa kutoka jijini Dar es Salaam mpaka mkoani Morogogro kwa usafiri wa h elkopta iliyotua katika viwanja vya Gymkhana.
 

Sheikh Ponda akiondoka mahakamani  baada ya kusomewa matatu na kesi yake imeahirishwa hadi tarehe 28/8/2013.

 

Ulinzi ukiwa umeimarishwa mahakamani hapo leo
Previous
Next Post »